Tarehe 19 Novemba, Chama cha CPC Shina la Wizara ya Elimu limeteua Bw. Li Hai kuwa Katibu Mtendaji wa CPC shina la BFSU na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo. Naibu Waziri wa Elimu Prof. Wang Jiayi amehudhuria kwenye mkutano na kutangaza uteuzi huo. Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Rasilimali Watu ya Wizara ya Elimu Bw. Ge Yuanjie, Naibu Katibu Mtendaji wa Baraza la Elimu la Beijing Bw. Yu Chengwen na Mkuu wa ...
Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing(BFSU) kimeandaa video fupi zinazoonesha maendeleo ya China katika Zama Mpya. Video hizi zinafuatilia masuala ya uhalisia na usasa kama vile malipo kwa njia ya simu, huduma ya kidijitali ya vyakula, ustawishaji wa vijijini, mawasiliano ya kitamaduni, huduma ya upelekaji wa vyakula, baiskeli za umma n.k. Lugha za video hizo ni pamoja na Kichina, Kiingereza, ...
Tarehe 27 Machi, Balozi wa Cambodia Nchini China Bi. Soeung Rathchavy ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian amekutana na wageni. Wamezungumza kuhusu kutayarisha wanafunzi na wasomi wa ngazi ya juu na kukuza ushirikiano wa utafiti na utamaduni.Kwa niaba ya Mama Malkia Monineath wa Cambodia, Balozi Rathchavy amezawadia BFSU vitabu. Jia Wenjian amepokea vitabu kwa niaba ya Chuo ...
Tarehe 17 Machi, Mwalimu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Keele Prof. Kevin Shakesheff na Makamu Mkuu Prof. Antonius Raghubansie wametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian na Makamu Mkuu Prof. Zhao Gang wamekutana na wageni hawa. Wamezungumza kuhusu kuimarisha miradi ya elimu ya ushirika ikiwemo shahada ya kwanza ya masomo ya diplomasia na shahada ya uzamili ya teknolojia ya elimu na akili ...
Tarehe 6 Machi, tafrija ya kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani imefanyika mjini Beijing. Mjumbe wa Baraza la Serikali na Mwenyekiti wa Shirikisho la Wanawake la China Bi. Shen Yiqin ametoa hotuba. Baadhi ya wawakilishi wanawake wa Bunge la Umma la China na wajumbe wa Baraza la Mashauriano ya Kisiasa la China, wanawake mashuhuri wa makabila na nyanja mbalimbali, wanawake kutoka Hong Kong na Macao, ...
Mnamo tarehe 28 Februari, kikao cha kufungua muhula wa Spring wa 2026 kimefanyika BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Bw. Li Hai, Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Jia Wenjian wamepanga kazi za mwaka mpya.Li Hai amesisitiza kuzingatia kazi muhimu zikiwemo “ufundishaji wa lugha, utafiti wa utamaduni na uwezo wa uongozi”, pamoja na kuendeleza ushirikiano wa ngazi ya juu na wa kila aina na vyuo vikuu maarufu ...
Tarehe 4 Februari, Rais wa Uruguay Mhe. Yamandu Orsi ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Bw. Li Hai, Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Jia Wenjian, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Zhao Gang, pamoja na Balozi wa China nchini Uruguay Bw. Huang Yazhong, Mwambata wa Idara ya Amerika ya Kilatini na Caribbean ya Wizara ya Mambo ya Nje Bw. Zhang Wenwei, Naibu Mkuu wa Idara ya Ushirikiano ...
Tarehe 24 Desemba, Balozi wa Uruguay nchini China Bw. Aníbal Cabral ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Jia Wenjian na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Zhao Gang wamekutana na wageni.Prof. Jia ameeleza habari za maendeleo ya taaluma, mawasiliano ya kimataifa na ujenzi wa kozi ya Kihispania wa BFSU. Amesema Chuo Kikuu cha BFSU kinazingatia sana mawasiliano na nchi za Amerika ya ...
Tarehe 12 Desemba, Balozi wa New Zealand nchini China Bw. Jonathan Austin ametemelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Bw. Li Hai amekutana na wageni. Wamezungumzia mawasiliano ya walimu na wanafunzi, utafiti wa pamoja, ujenzi wa kozi za Kimaori na lugha nyingine za Kusini mwa Pasifiki.