Tarehe 30 Januari, sherehe ya mwaka mpya ya walimu wa kigeni imefanyika katika Chuo Kikuu cha BFSU. Walimu wote wa kigeni wa BFSU na familia zao, wawakilishi wa walimu na wanafunzi zaidi ya 100 wameshiriki sherehe hiyo. Makamu Mkuu Prof. Zhao Gang ametoa risala kwenye sherehe na kuwatakia heri na fanaka. Walimu wanne waliofundisha zaidi ya miaka 10 katika BFSU wametunukiwa tuzo. Prof. Charassri Jiraphas ...
Mnamo tarehe 17 hadi 18 Desemba, Kongamano la Nane la Kiswahili la Kimataifa limefanyika Pemba, Zanzibar. Zaidi ya wasomi 150 wanaotoka nchi 10 wameshiriki kwenye Kongamano hilo.Mwanafunzi wa shahada ya uzamili wa BFSU Bw. Qin Zulong ameshiriki Kongamano hilo akiwasilisha ripoti inayochambua makosa ya kisarufi ya wanafunzi wa Kiswahili wa China katika mchakato wa upatanishi.Qin amezungumza na wasomi ...
Kuanzia tarehe 14 hadi 23 Desemba, Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Jia Wenjian ameongoza ujumbe kutembelea Saudi Arabia, Misri na Algeria. Wajumbe hawa wametembelea Chuo Kikuu cha Mwana wa Mfalme Sultan na Chuo Kikuu cha Binti wa Mfalme Nourah Bint Abdulrahman nchini Saudi Arabia, Chuo Kikuu cha Ain Shams, Chuo Kikuu cha Badr nchini Misri na Chuo Kikuu cha Algiers III nchini Algeria kwa ajili ya ...
Tarehe 18 Novemba, Kongamano la Taasisi za Confucius za BFSU limefanyika katika Chuo Kikuu cha BFSU. Kongamano hilo lenye kaulimbiu ya “Kufunzana na Kuandika Sura Mpya ya Maendeleo ya Taasisi za Confucius kwa Pamoja” limelenga kuimarisha mawasiliano na kuhimiza maendeleo ya daraja la juu ya taasisi hizo. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian ameshiriki kwenye ufunguzi wa Kongamano. Wakurugenzi na viongozi ...
Kuanzia tarehe 15 hadi 17 Novemba, Mkutano wa Kimataifa wa Lugha ya Kichina 2024 umefanyika jijini Beijing. Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Mawasiliano na Mwingiliano, Urithi na Ubunifu”. Zaidi ya wasomi, wataalamu, mabalozi na wawakilishi 2,000 wa asasi za elimu, vyuo vikuu, makampuni na mashirika ya kimataifa kutoka nchi na kanda zaidi ya 160 wamehudhuria mkutano huo. Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof....
Tarehe 28 Oktoba, Mshauri wa Chuo Kikuu cha Chicago Prof. John Boyer ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU na kutoa mhadhara wenye mada ya “Historia na Maendeleo ya ‘Elimu ya Kibinadamu’: Mfano wa Chuo Kikuu cha Chicago”. Mwenyekiti wa Baraza la BFSU Prof. Wang Dinghua amekutana na mgeni huyo na msafara wake.
Tarehe 25 Oktoba, Mkuu wa Chuo Kikuu cha Katoliki cha Uruguay Prof. Julio Fernández Techera ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian amekutana na mgeni huyo. Pande hizo mbili zimezungumia kuhusu utafiti wa Amerika ya Kilatini, uhusiano wa China na Amerika ya Kilatini, mawasiliano ya walimu na wanafunzi na masuala mengine.
Kuanzia tarehe 6 hadi 8 Oktoba, Kongamano la Viongozi wa Kimkakati wa Dunia la 2024 limefanyika mjini Guadalajara nchini Mexico. Kwa kufuata mwaliko wa Baraza la Shule za Shahada ya Uzamili na Uzamivu la Marekani, Mkuu wa Jumuiya ya Elimu ya Shahada ya Uzamili na Uzamivu ya China Bw. Yang Wei ameongoza ujumbe kuhudhuria kongamano hilo. Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Jia Wenjian ameshiriki na kutoa ...
Tarehe 11 Oktoba, Spika wa Cyprus Bi. Annita Demetriou ameongoza ujumbe kutembelea Chuo Kikuu cha BFSU na kutoa hotuba. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian amemkaribisha. Baada ya kutoa hotuba, Bi. Demetriou amezungumza na kujibu maswali ya walimu na wanafunzi wa BFSU.