Tarehe 11 hadi 13 Mei, Mkutano wa Nane wa Ushirikiano wa Elimu wa China na Belarusi, Baraza la Kwanza la Mawaziri wa Elimu wa China na nchi za Asia ya Kati, kikao cha mwaka 2025 cha vyuo vikuu wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai(SCO), Baraza la Tisa la Mawaziri wa Elimu la SCO vimefanyika Urumqi, Xinjiang. Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Jia Wenjian amehudhuria mikutano hiyo. Tarehe 11, Mkutano ...
Tarehe 16 hadi 24 Aprili, mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Jia Wenjian ameongoza ujumbe kutembelea Kazakhstan, Uzbekistan na Kyrgyzstan. Wajumbe hawa wametembelea Chuo Kikuu cha Taifa cha Al-Farabi Kazakh, Chuo Kikuu cha Mahusiano ya Kimataifa na Lugha za Dunia cha Kazakh Ablai Khan, Chuo Kikuu cha Nazarbayev, Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Utalii na Masalio ya Kitamaduni ya “Ukanda Mmoja, Njia Moja”...
Tarehe 9 Aprili, sherehe ya kutia saini makubaliano ya ushirikiano wa Chuo Kikuu cha BFSU na SOAS imefanyika SOAS, London. Naibu meya wa mji wa Beijing Bw. Ma Jun amehudhuria sherehe hiyo na kutoa hotuba. Makamu mkuu wa BFSU Prof. Zhao Gang na makamu mkuu wa SOAS Prof. Laura Hammond wametia saini makubaliano hayo.
Tarehe 11 Aprili, balozi wa Sri Lanka Bw. Majintha Jayesinghe ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian amekutana na wageni hawa. Wamezungumzia kuimarisha ushirikiano wa BFSU na Sri Lanka katika mawasiliano ya walimu na wanafunzi, utafiti wa pamoja na mengineyo.
Tarehe 13 Aprili, balozi wa Malta nchini China Bw. John Busuttil na mkuu wa Chuo Kikuu cha Malta Prof. Alfred Vella wametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian, makamu mkuu wa BFSU Prof. Liu Xinlu wamekutana na wageni hawa na kuzungumzia kuimarisha ushirikiano.Wageni hao wamekutana na wanafunzi wa Kimalta kabla ya mazungumzo.
Tarehe 16 Aprili, balozi wa Uswidi nchini China Bw. per Augustsson ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua amekutana na wageni hawa. Wamezungumzia kuimarisha ushirikiano kati ya BFSU na pande za Uswidi, kuendeleza mawasiliano ya walimu na wanafunzi na kukuza utafiti. Kabla ya kukutana na viongozi wa BFSU, Bw. Augustsson amefanya mazungumzo na walimu na ...
Tarehe 25 Machi, Waziri wa mambo ya ndani na nje wa Ureno Bw. Paulo Rangel ametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mkuu wa BFSU Prof. Jia Wenjian amekutana na wageni hawa. Bw. Rangel ametoa hotuba kuhusu lugha na utamaduni wa Ureno kabla ya kuzungumza na walimu na wanafunzi wa Kireno.
Tarehe 20 hadi 29 Machi, mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Wang Dinghua ameongoza ujumbe kutembelea Austria, Uswisi na Ureno. Wajumbe hawa wametembelea Kituo cha Utafiti cha Jellinek cha Austria, Chuo Kikuu cha Vienna na taasisi yake ya Confucius, Taasisi ya Mahusiano ya Kimataifa na Maendeleo ya Geneva, Chuo Kikuu cha Porto, Chuo Kikuu cha Coimbra na Chuo Kikuu cha Lisbon.Wajumbe hao ...
Tarehe 22 Machi, Baraza la Tisa la Mageuzi na Maendeleo ya Elimu ya Lugha za Kigeni katika Vyuo Vikuu limefanyika Beijing. Jukwaa la Huduma ya Lugha la Dunia limezinduliwa katika baraza hilo. Kwa kufuata dhamira ya kujenga, kuzalisha na kutumia kwa pamoja, Jukwaa hilo limeweka vitengo vitatu vya huduma ya lugha , elimu ya lugha na utafiti na hifadhi ya lugha.