Tarehe 12 Machi, Mkuu wa SOAS Bw. Adam Mohamed Habib na msafara wake wametembelea Chuo Kikuu cha BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Jia Wenjian wamekutana na wageni hawa.Prof. Wang Dinghua ameeleza habari za maendeleo ya taaluma na mawasiliano ya kimataifa ya BFSU, na ametumai kuimarisha ushirikiano kati ya pande mbili katika kuendeleza ...
Mnamo tarehe 28 Februari, kikao cha kufungua muhula wa Spring wa 2024 kimefanyika BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua amepanga kazi za muhula huu kwa pande zote.Prof. Wang Dinghua ameweka wazi mambo kumi ya kufanya. Kwanza, kutathmini na kukuza elimu ya shahada ya kwanza kwa vigezo vizuri. Pili, kupanga mikakati ya maendeleo ya taaluma. Tatu, kuharakisha ujenzi wa “Chuo...
Mnamo tarehe 6 Januari, Mazungumzo ya Diplomasia ya umma kati ya China na Ulaya yamefanyika Beijing. Mazungumzo hayo yameandaliwa na Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing na Taasisi ya Taaluma za Utawala wa Kanda na Dunia. Zaidi ya watu 100 kutoka serikali, vyuo vikuu, wataalamu, waandishi wa habari wameshiriki mazungumzo hayo. Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan amehudhuria na kuto...
Kuanzia tarehe 7 hadi 9 Desemba, Mkutano wa Kimataifa wa Lugha ya Kichina umefanyika Beijing. Kaulimbiu ya mkutano huo ni “Kuhudumia Dunia kwa Kichina, Kufungua Mlango kwa Mustakabali”. Zaidi ya wasomi, wataalamu, maafisa wa serikali na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa 2,000 wamehudhuria mkutano huo. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Wang Dinghua, Makamu Mkuu wa Chuo Prof...
Kuanzia tarehe 1 hadi 10 Desemba, Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan ameongoza wajumbe kutembelea Ethiopia, Madagaska na Tanzania. Wametembelea Chuo Kikuu cha Addis Ababa, Chuo Kikuu cha Antananarivo, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kutia saini makubaliano ya ushirikiano baada ya mazungumzo na wakuu wa vyuo husika. Zaidi ya hayo, Prof. Yang Dan na wajumbe wametembelea makampuni ya China...
Mnamo tarehe 18 Novemba, Kongamano la “Bazara: Swahili Studies Conference 2023” limefanyika katika London, Uingereza. Zaidi ya wasomi 50 wanaotoka nchi mbalimbali wameshiriki katika kongamano hilo.Mwanafunzi wa shahada ya uzamili wa BFSU Bw. Ding Ruilin ameshiriki katika kongamano hilo akiwasilisha ripoti inayochambua athari hasi za tafsiri kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili katika fasihi za ...
Kuanzia tarehe 9 hadi 17 Novemba, Mwenyekiti wa Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua ameongoza wajumbe kutembelea Argentina, Brazil na Costa Rica. Wametembelea vyuo vikuu mbalimbali katika nchi hizo na kusaini makubaliano ya ushirikiano ili kuimarisha ushirikiano wa elimu na utafiti, kuongeza ajira kwa wanafunzi na kuchunguza njia mpya ya kuendeleza Taasisi za Confucius. Pia wametembelea Ubalozi wa Ch...
Mnamo tarehe 23 Oktoba, Mkurugenzi Mkuu wa Zamani wa UNESCO Bi. Irina Bokova, ametembelea BFSU na kutoa hotuba yenye mada ya "Utamaduni na Utawala wa Ulimwengu". Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan amehudhuria mhadhara na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Zhao Gang ameendesha mhadhara huo.Bi. Bokova amefafanua uhusiano uliopo kati ya utamaduni na maendeleo endelevu akielezea uzoefu wa Umoja wa M...
Mnamo tarehe 17 Oktoba, Katibu wa Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ya Kambodia Bw. Lau Vann ametembelea BFSU. Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan amekutana na Bw. Lau Vann na msafara wake, wamebadilishana mawazo juu ya mawasiliano na ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.
Mnamo tarehe 17 Oktoba, Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan amekutana na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Ali Farabi cha Kazakhstan Bw. Tuimebayev Zhanseit Kanseituly katika Kongamano la Tatu la Ushirikiano wa Kimataifa wa "Ukanda Mmoja, Njia Moja". Pande hizo mbili zimetia saini mkataba wa kupelekeana wanafunzi wa vyuo vikuu viwili.
Mnamo tarehe 17 Oktoba, Mke wa Rais wa Sri Lanka Prof. Maithree Wickremesinghe ametembelea BFSU na kutoa hotuba. Pia amekutana na walimu na wanafunzi zaidi ya 300 wanaotoka vitivo mbalimbali. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua amehudhuria sherehe hiyo na kutoa risala.
Mnamo tarehe 27 Septemba, Waziri waUchukuzi na Vyombo vya Habari na Msemaji wa Baraza la Mawaziri la Sri Lanka Bw. Bandula Gunawardena ametembelea BFSU. Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Jia Wenjian wamekutana na Bandula na ujumbe wake. Wamebadilishana mawazo juu ya kuendelea kuimarisha mawasiliano na ushirikiano katika mafunzo ya wanafunzi wa lugha ya Kisi...
Mnamo tarehe 26 Septemba, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Syria Bi. Asma al-Assad ametembelea BFSU na kutoa hotuba kwenye Ukumbi wa Mkutano wa Kimataifa wa Kitivo cha Kiarabu. Pia amekutana na wawakilishi 40 kutoka balozi, vyuo vikuu na taasisi za utafiti. Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Jia Wenjian amehudhuria hafla hiyo na kutoa risala.
Mnamo tarehe 22 Septemba, Kongamano la Mawasiliano ya Kimataifa ya Utamaduni wa China limefanyika Beijing. Kongamano hilo liliandaliwa na Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing, Shirika la Uchapishaji wa Kimataifa la China na Taasisi ya Utamaduni wa China. Mada ya kongamano hili ni “Tekeleza Mipango ya Ustaarabu wa Kimataifa na Kukuza Maendeleo ya Ustaarabu wa Binadamu kwa Pamoja ”. Takri...
Mnamo Septemba 16, Kongamano la Ustaarabu wa Ulimwengu limefanyika katika Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing. Kaulimbiu ya kongamano ilikuwa “Kuwasiliana na Utamaduni wa Ulimwengu ili Kuongeza Uelewa wa Kimataifa”. Zaidi ya watu 600 kutoka serikalini, vyuo vikuu vya ndani na nje ya nchi, wataalamu, wanafunzi na walimu wa BFSU wameshiriki kongamano hilo. Kongamano hili linakusudia kush...
Mnamo Septemba 4, sherehe ya kuwakaribisha wanafunzi wapya wa 2023 imefanyika hapa Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing. Kwa ujumla, wanafunzi wapya 3,267 wamejiunga na chuo hiki na kuanza maisha mapya.Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua, Mkuu wa Chuo Kikuu cha BFSU Prof. Yang Dan na aliyekuwa Naibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano ya Kimataifa ya Kamati Kuu ya Chama cha Ki...
Tarehe 31 Agosti 2023, Jumuiya ya Elimu ya Juu ya China (CAHE) na Jumuiya ya Vyuo Vikuu vya Afrika (AAU) zimezindua Sekretarieti ya China ya Umoja wa Vyuo Vikuu vya China na Afrika katika BFSU.Mkuu wa CAHE Bw. Du Yubo, Makamu Mkuu wa CAHE Bw. Zhang Daliang, Katibu Mkuu wa AAU Prof. Olusola Oyewole na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua wamehudhuria sherehe ya uzinduzi huo.Chin...