Mnamo tarehe 6 Juni, Mwenyekiti wa Chama cha SPD cha Ujerumani Bw. Lars Klingbeil ameongoza ujumbe kutembelea Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing (BFSU) na kutoa hotuba. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua na Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Jia Wenjian wamekutana na Klingbeil na msafara wake. Bw. Klingbeil ametoa hotuba yenye mada ya "The Changing World Order" na kujibu maswali ya walimu na wanafunzi wa BFSU.