CHUO KIKUU CHA LUGHA

ZA KIGENI, BEIJING

Miradi Mikuu Mitano ya NSSFC ya BFSU Yaidhinishwa

发布时间:2022-01-03

Hivi karibuni, orodha ya miradi mikuu ya NSSFC ya mwaka 2021 imetolewa. Miradi minne ya BFSU imeidhinishwa ikishika nafasi ya 21 kati ya vyuo vikuu kote nchini. Mradi wa "Uhariri na utafiti wa vitabu vya kiada vya lugha za kigeni katika vyuo vikuu: Kuelewa China ya Kisasa" ukiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof.Wang Dinghua umeidhinishwa kuwa mradi mkubwa wa NSSFC.

Kabla ya hapo, miradi 16 ya BFSU iliidhinishwa na NSSFC mwaka 2021, miradi 5 iliidhinishwa na Taasisi ya Kitaifa ya Sayansi ya China, miradi 10 iliidhinishwa kuwa miradi ya utafiti wa sanaa na sayansi ya jamii ya Wizara ya Elimu, na miradi 5 iliidhinishwa kuwa miradi ya Mfuko wa Sayansi ya Jamii mjini Beijing. Miradi hiyo imejumuisha nyanja mbalimbali kama vile isimu, fasihi, uandishi wa habari, utafiti wa masuala ya kimataifa na kadhalika.


Orodha ya Miradi Mikuu ya NSSFC ya BFSU iliyoidhinishwa mwaka 2021

Nambari

Majina ya Miradi

Nambari ya kuidhinishwa

Mtaalamu mkuu

1

Uhariri na utafiti wa vitabu vya kiada vya lugha za kigeni katika vyuo vikuu: Kuelewa China ya Kisasa

21@ZH043

Wang Dinghua

2

Utafiti wa ushawishi wa kimataifa wa istilahi kuu za China

21&ZD158

Yuan Jun

3

Utafiti juu ya Ukuzaji na Utumiaji wa Makundi Makubwa Sambamba ya Lugha mbalimbali za Kichina-Kigeni

21&ZD290

Wang Kefei

4

Utafiti wa Mfumo wa Kawaida, Tathmini na Uingiliaji kati wa Uwezo wa Lugha wa Wazee nchini China

21&ZD294

Gu Yueguo

5

Utafiti juu ya Uenezaji na Utambuzi wa Kimataifa wa Taswira ya Chama cha Kikomunisti cha China chini ya Mabadiliko Makubwa Yasiyo na Kifani Katika Karne Iliyopita.

21&ZD314

Gao Jinping





No. 2 North Xisanhuan Road, Beijing, P.R.China. (100089)

OFFICE FOR INTERNATIONAL EXCHANGE AND COOPERATION

OFFICE OF CONFUCIUS INSTITUTES

OFFICE FOR OVERSEAS STUDENTS AFFAIRS

GENERAL ADMINISTRATION OFFICE

Copyright@BFSU.Support by ITC