Mnamo Julai 2, Mahafali ya mwaka 2021 ya Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing yamefanyika hapa chuoni. Mwaka huu, wanafunzi 2,197 wametunukiwa shahada ya kwanza, wanafunzi 1,064 wametunukiwa shahada ya uzamili na wanafunzi 61 wametunukiwa shahada ya uzamivu. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua na Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Yang Dan waliwapa wahitimu pongezi na kuwatunukia cheti chao.