Mnamo tarehe 28 Februari, kikao cha kufungua muhula wa Spring wa 2026 kimefanyika BFSU. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Bw. Li Hai, Mkuu wa Chuo Kikuu Prof. Jia Wenjian wamepanga kazi za mwaka mpya.

Li Hai amesisitiza kuzingatia kazi muhimu zikiwemo “ufundishaji wa lugha, utafiti wa utamaduni na uwezo wa uongozi”, pamoja na kuendeleza ushirikiano wa ngazi ya juu na wa kila aina na vyuo vikuu maarufu duniani, ili kuboresha ubora na ufanisi wa kuendeleza elimu ya ushirika. Pia amesisitiza kuendeleza ujenzi wa Taasisi za Confucius na miradi maalumu kama “Daraja la Kichina” ili kuongeza ushawishi wao. Jia Wenjian amesisitiza umuhimu wa kuendeleza elimu ya ushirika na SOAS, kujenga jukwaa jipya la Taasisi za Confucius na kuendeleza mradi wa “Kusoma nchini China”.