Mnamo Julai 5, Sherehe ya Uzinduzi wa Seminaya Kimataifa ya Siku za Joto ya mwaka 2021 ilifanyika kwa njia ya mtandao. Walimu 13 wa kigeni waliotoka ulimwenguni walijitambulisha kupitia matangazo ya moja kwa moja na video zilizorekodiwa. Mwaka huo, maprofesa 13 wamealikwa kutoa mafunzo ya fani zikiwemo isimu, sayansi ya kisiasa, sosholojia, uchumi, historia, mahusiano ya umma, maendeleo ya maeneo, masomo ya mawasiliano, fasihi na sanaa. Kwa ujumla, wanafunzi 181 wamejiunga na semina ya mwaka huo.
