HOME > Habari > Content

Balozi wa UAE atembelea BFSU

Updated: 2023-05-10

Mnamo tarehe 4 Mei, Balozi wa Umoja wa Falme za Kiarabu nchini China Bw. Ali Obaid Al Dhaheri ametembelea Chuo Kikuu cha Lugha za Kigeni cha Beijing. Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Prof. Wang Dinghua amekutana na Bw. Dhaheri na msafara wake. Wamejadiliana juu ya kuimarisha ushirikiano katika kupelekeana wanafunzi, mafunzo ya pamoja na mawasiliano ya kitaaluma. Baada ya mkutano, Bw. Dhaheri amefanya mazungumzo na walimu na wanafunzi wa BFSU.