Tarehe 20 Machi, maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Lugha ya Kifaransa yamefanyika kwenye Ubalozi wa Ufaransa nchini China. Wizara ya Elimu ya Ufaransa imemtunukia Mkuu wa Kitivo cha Kifaransa cha BFSU Prof. Dai Dongmei tuzo ya Academic Palm Knight kwa kuzingatia mchango wake katika kuendeleza elimu ya Kifaransa na kueneza utamaduni wa Kifaransa. Balozi mpya wa Ufaransa nchini China Bw. Bertrand Lortholary amemtunukia Prof. Dai Dongmei nishani hiyo.